Ikiwa una Taarifa yoyote kuhusiana na Komedi, tangazo, Filamu mpya na mengineyo tuma kupitia Whatsapp namba +255653146563 au +255765056399  
Na Vijimambo
Mhubiri wa kimataifa na mchekeshaji maarufu Emmanuel Mgaya au jina 
maarufu Masanja Mkandamizaji juzi alitembelea studio za kuzalisha muziki
 na video za SamSPRO Studios zilizoko Washington, DC.
Masanja kama anavyoonekana kwenye picha aliambatana na waimbaji wa 
nyimbo za injili Milca Kakete kutoka Canada na Milca Thomas kutoka North
 Carolina, pamoja na baadhi ya waimbaji wa kundi la The Sound of Glory 
kutoka kanisa la The Way of the Cross Gospel Ministries lililoko 
Washington DC ambako mwigizaji huyo maarufu alikuwepo kama mhubiri mkuu 
wa mkutano uliokuwa ukiendelea kwa siku tatu mfululizo. 
Akijibu swali alipoulizwa juu ya ugeni huo studioni hapo producer na 
mmiliki wa studio hiyo ndugu Samuel Malonja alisema kuwa Masanja aliamua
 kutafuta studio ambayo anaweza kuitumia kurekodi wimbo wake, hilo ndio 
lilikuwa lengo la ugeni huo.
Masanja amerekodi wimbo mmoja katika studio hiyo akiwashirikisha 
waimbaji wengine wa injili akiwemo Milca Kakete kutoka Canada, Milca 
Thomas kutoka North Carolina na waimbaji wa kanisa la The Way of the 
Cross Gospel Ministries la mjini Washington DC.
Picha hapo chini zinaonyesha kazi ya kurekodi wimbo huo chini ya 
producer Sam ikiendelea huku Masanja akionekana kusimamia zoezi hilo kwa
 umakini kabisa.







No comments:
Post a Comment