Social Icons

Pages

Tuesday, June 2, 2015

EXCLUSSIVE STORY:UKWA WA BONGO MUVI ASHEREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA UGALI WA MUHOGO, SAMAKI NA KACHUMBALI...

Ikiwa una Taarifa yoyote kuhusiana na Komedi, tangazo, Filamu mpya na mengineyo tuma kupitia Whatsapp namba +255653146563 au +255765056399 


 Ukwa wa Bongo Movie akiwa na mama yake
Huu ndio msosi na mahanjamu

Msanii wa komedi, Nicholaus Ngoda a.k.a Ukwa wa Bongo Muvi amejikuta akisherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa majonzi baada ya afya ya mama yake mzazi kudorora hali iliyomlazimu akatishe mipango ya kuangusha pati kwa ajili ya siku hiyo kama alivyopania.

Kamera ya Komedi Zone ilimnasa msanii huyo Juni 1 mwaka huu nyumbani kwa mama yake maeneo ya Kiwalani Bombomu jijini Dar alipoenda kumtembelea ambapo msanii huyo alimua kusherehekea siku hiyo kwa kumuangushia msosi wa ‘kinyumbaninyumbani’ mama yake mzazi aliyemtambulisha kwa jina la Agnes George.

“Dah kaka siku yangu ya kuzaliwa ilijaa huzuni kidogo mama yangu anaumwa hivyo nilienda kumtembelea na nikafanyia sherehe kwake,tena sikutaka keki wala nini tulikula ugali wa mhogo, samaki wakukaanga, kachumbali na bamia za kuunga, in short nilifurahia sana kusherehekea na mama yangu,” alisema Ukwa. 

NA KOMEDI ZONE

No comments:

Post a Comment