Msanii wa
Komedi, Morgan Ngoda maarufu kama ‘Ukwa wa Bongo’, amesimulia jinsi kazi yake
ya kuigiza ilivyovunja penzi lake na mchumba wake wa siku nyingi aliyepanga
kumuoa.
Akipiga
stori na mwandishi wetu, Ukwa alisema kuwa akiwa katika michakato ya
kutambulishana kwa ajili ya kukamilisha taratibu za uchumba, wazazi wa mpenzi
wake walitaka kujua kazi yake ndipo alipowaambia kuwa ni msanii wa Bongo Muvi,
jambo lililowachefua wakwe hao waliodai Bongo Muvi imejaa ufuska na hafai
kumuoa msichana huyo.
“Yaani wale
wazazi hawakukubali kabisa utetezi wangu walinidai moja kwa moja kuwa mimi ni
kama wenzangu wa Bongo Muvi, wakanitaka nikae mbali na mtoto wao, na kweli
kuanzi siku hiyo mimi na mipango ya kuoa basi tena,” alisema Ukwa.
Ikiwa una Taarifa yoyote kuhusiana na Komedi, tangazo, Filamu mpya na mengineyo tuma kupitia Whatsapp namba +255653146563 au +255765056399
No comments:
Post a Comment