Mchekeshaji maarufu kutoka bongo jacob Mkweche a.k.a. Ringo amefungukia kuhusu kuendelea kuuzwa cd za bukubuku kuwa kunadidimiza uchumi wao na kwa Taifa kwa ujumla.
Akizungumza na Komedi Zone Ringo amesema licha ya kuwa kuonesha vipaji vyao kwa mashabiki lakini hali ya kimaisha waliokuwa nayo haifanani na majina walikuwa nayo.
Aidha pia amefafanua kuwa baadhi ya wasambazaji wa filamu wamekuwa hawathamini kazi yao hata kidogo kwa kuwanyonya kwa kuuza filamu zao kwa bei chee kitu ambacho kinawaporomosha kimaisha.
"Ninaiomba serikali kuingilia katika swala hili vinginevyo mafanikio tutasikia kwenye bomba," alisema Ringo
"Ninaiomba serikali kuingilia katika swala hili vinginevyo mafanikio tutasikia kwenye bomba," alisema Ringo
Na Komedi Zone
No comments:
Post a Comment