Social Icons

Pages

Tuesday, May 19, 2015

MTANGA: NAOGOPA KUIBIWA NIKIMWEKA HADHARANI MKE WANGU


Msanii wa Komedi Bongo, Hamisi Kihangare ‘Mtanga’ amefunguka kuwa anahofu kumweka hadharani mkewe hasa kwenye mitandao kwa kuwa anaogopa kuibiwa na kusumbuliwa na wanaume wakware.

Akipiga stori na paparazi wetu wa Komedi Zone, Mtanga alisema kuwa ataishia kuwaweka mtandaoni watoto wake Nadya na Shadya, lakini si kwa mama yao ambaye aligoma kumtaja jina lake wala kuonesha picha yake kwa kuhofia kuwarahisishia watu kumpata.

“Wewe tambua tu kwamba mke wangu anaitwa Mama Shadya, jina lake halisi na picha yake sitoa si unajue naogopa watu nitawarahisishia kumsumbua kirahisi jambo ambalo naogopa sana,” alisema Mtanga.  

Na Komedi zone.

No comments:

Post a Comment